Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/personal/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Kwa nini vijana wanakatazwa kujamiiana?

Featured Image

Ujana ni kipindi cha mabadiliko kutoka utotoni kuelekea utu uzima, wakati wa kipindi hiki kijana hupata mabadiliko ya kimwili, kiakili na kimtazamo. Mwili na akili hupevuka. Ni kipindi muhimu cha kuweka msingi wa maisha ya baadaye. Vijana wanakatazwa kujamiiana kwa sababu matatizo mengi yanaweza kutokea kutokana na tendo hilo.

Kwanza kabisa kwa kujihusisha na kitendo cha kujamiiana vijana wanapoteza nguvu na muda ambao wangeweza kutumia kwa shughuli za maendeleo. Kwa mfano, kusoma, kufanya kazi, kushiriki katika shughuli za vikundi katika jamii au kucheza michezo.
Pili, matatizo ya mimba katika umri mdogo ni mengi. Mojawapo ni msichana kufukuzwa shule, au hata jamii kumtenga. Matatizo mengine ni ya kiafya kutokana na mwili wa msichana bado kuwa haujakomaa vyema.
Tatu, vijana wanakuwa bado hawajajiandaa kwa uzazi au kujitegemea. Sababu nyingine ya kuwakataza vijana kujamiiana ni ile ya hatari ya kuambukizana magonjwa ya zinaa ikiwa ni pamoja na Virusi vya UKIMWI. Magonjwa haya ni mabaya sana yanaweza kusababisha maumivu makali, ugumba au hata kifo.
Unapofikiria sababu zote hizo utaona kwamba kujamiiana katika umri mdogo kunaweza kuleta madhara mengi kwa afya yako na malengo yako maishani. Hivyo basi unapokatazwa kujamiiana ni kwa sababu ya matatizo haya. Hata hivyo, kama kwa vyovyote huwezi kuacha kujamiiana, hakikisha kwamba unajikinga wewe na mpenzi wako kwa kutumia kondomu.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Je, watu wana amini katika kutumia mbinu za kujizuia mimba wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wana amini katika kutumia mbinu za kujizuia mimba wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Salamu! Karibu kwenye makala ya leo kuhusu mbinu za kujizuia mimba wakati wa ngono. Ni jambo muhi... Read More

Je, kuna madhara kama mtu akikaa muda mrefu bila kufanya mapenzi?

Je, kuna madhara kama mtu akikaa muda mrefu bila kufanya mapenzi?

Ukweli ni kwamba hakuna madhara yoyote ya kiafya ukikaa muda mrefu bila kujamii ana. Hakuna madha... Read More

Je, magonjwa ya zinaa yanaweza kuenea ukitoa uume kabla ya kumwaga mbegu?

Je, magonjwa ya zinaa yanaweza kuenea ukitoa uume kabla ya kumwaga mbegu?

Ndiyo, magonjwa ya zinaa yanaweza kuenea, hata ukitoa uume kabla ya kumwaga mbegu. Mwenye magonjw... Read More

Jinsi ya Kuwa na Tarehe ya Ushirikiano na Msichana

Jinsi ya Kuwa na Tarehe ya Ushirikiano na Msichana

  1. Anza kwa Kujijenga Kimaumbile Kabla ya kumwomba msichana tarehe ya ushirikiano, ni muhi... Read More

Jinsi ya Kuonyesha Utambulisho Wako kwa Msichana

Jinsi ya Kuonyesha Utambulisho Wako kwa Msichana

Jinsi ya Kuonyesha Utambulisho Wako kwa Msichana

Kuonyesha utambulisho wako kwa msichana n... Read More

Jinsi mimba inavyopatikana

Jinsi mimba inavyopatikana

Ukitaka kuelewa jinsi mimba i inavyopatikana, lazima uelewe mzunguko wa hedhi wa mwanamke. Baada ... Read More

Je, Ni Sahihi Kutumia Dawa za Kuzuia Mimba?

Je, Ni Sahihi Kutumia Dawa za Kuzuia Mimba?

Je, Ni Sahihi Kutumia Dawa za Kuzuia Mimba? 🌼😊

Tunaelewa kwamba vijana wetu ni kikun... Read More

Lengo na sababu ya kujamiiana

Lengo na sababu ya kujamiiana

Lengo kuu la kujamiiana ni kutafuta watoto. Lakini si sababu pekee. Sababu hizo ni pamoja na;

... Read More
Njia Rahisi za Kufanya Msichana Awe na Hamu ya Kuwa na Wewe

Njia Rahisi za Kufanya Msichana Awe na Hamu ya Kuwa na Wewe

Wapenzi, kama unapenda msichana fulani na unataka kuwa na uhusiano naye, inaweza kuwa ngumu kumsh... Read More

Vidokezo vya Kuwa na Mazungumzo ya Kusisimua na Msichana

Vidokezo vya Kuwa na Mazungumzo ya Kusisimua na Msichana

Kama mvulana, unajua kuwa mazungumzo na msichana yako yanaweza kuwa magumu sana. Unaweza kuwa na ... Read More

Sheria zinazohusiana na ndoa za kulazimishwa

Sheria zinazohusiana na ndoa za kulazimishwa

Sheria ya msingi ya ndoa nchini Tanzania ni Sheria ya ndoa ya
Bunge, iliyopitishwa mwaka 197... Read More

Je, watu wote wenye virusi vya UKIMWI watapata UKIMWI? Na kama ndiyo, itachukua muda gani?

Je, watu wote wenye virusi vya UKIMWI watapata UKIMWI? Na kama ndiyo, itachukua muda gani?

Ndiyo, baada ya muda fulani karibia watu wote wenye maambukizi ya Virusi vya UKIMWI wataanza kuug... Read More

πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About