Sababu ya tatizo la Tumbo kujaa gesi na jinsi ya kujitibu
Date: April 15, 2022
Author: SW - Melkisedeck Shine
Tatizo la tumbo kujaa gesi husababishwa na kumeza chakula pamoja na gesi inayotolewa katika vyakula mbalimbali tunavokula ambayo hujaa tumboni na kwenye utumbo mdogo. Hali hii husababisha tumbo kujaa au kuvimba na mtu hutoa gesi hiyo kwa njia ya ushuzi na kubeua.
Nini husababisha.
Tatizo ili mara nyingi husababishwa na huambatana na mambo yafuatayo:
1. Kula vyakula vyenye mafuta mengi ambayo huchelewesha tumbo kufunguka kwa ajili ya usagaji wa chakula.
2. Kunywa vinywaji vyenye Carbonates, cola na kula vyakula vyenye gesi kama maharage, bigiji, vitunguu, kabichi n.k
3. Msongo wa mawazo na hasira.
4. Kula haraka haraka na kula unaongea.
5. Uvutaji wa Sigara
6. Magonjwa na maambukizi katika mfumo wa chakula asa kwenye tumbo na utumbo ambayo huzuia kusagwa na kufyonzwa kwa chakula.
Jinsi ya kujitibu.
ยท Kunywa chai ya tangawizi au karafuu itasaidia kupunguza gesi.
ยท Unaweza kunywa glasi moja ya juisi ya Limao baada ya kula.
ยท Tafuna mbegu za maboga zinasaidia kulainisha mfumo wa chakula
ยท Lalia ubavu wa kushoto na pumua kwa kasi ili kupunguza gesi tumboni.
ยท Kunja miguu na ikalie uku ukinyoosha mikono na kuinamia mbele itasaidia.
ยท kuongeza kasi ya mfumo wa chakula kufanya kazi na kuondoa gesi.
ยท Fanya mazoezi mepesi ya kutembea na kuruka ruka.
ยท Kula na tafuna chakula taratibu na epuka vyakula vyenye gesi na mafuta mengi,.
ยท Nenda hospitali kama tatizo ili linaambatana na kuharisha, kutapika, maumivu makali ya tumbo, kinyesi chenye rangi tofauti au damu na maumivu ya kifua.
Please log in or register to leave a comment or reply.
Related Posts
Ulaji wa vyakula vingi vya wanga na mafuta ni chanzo kikubwa cha unene na uzito kuongezeka. Vyaku...
Read More
Ili kuongeza mbegu za kiume zingatia haya yafuatayo;
Kula lishe bora
Chakula unacho...
Read More
Kahawa husaidia kuongeza presha au shinikizo la damu. Unashauriwa Kunywa kikombe kimoja cha kahaw...
Read More
Unahitaji:
a)Kijiko kimoja cha asali
b)Parachichi 1
Hatua kwa hatua namna ya ...
Read More
Dawa nyingine nzuri kwa ajili ya chunusi usoni na mwilini ni limau. Limau linajitokeza kwenye vya...
Read More
Siku zote sisi wanadamu huwa tunaambizana kuwa, kinga ni bora kuliko tiba, tukiwa na maana kwamba...
Read More
Kwa ajili afya ya mama na mtoto ni muhimu sana, mwanamke anatakiwa apate chakula bora kilicho na ...
Read More
Unaweza kutumia Lozi na maziwa kutibu shinikizo la chini la damu kama ifuatavyo;
- Lowek...
Read More
BILA shaka ubongo ni miongoni mwa viungo muhimu vya binadamu lakini ni watu wachache sana wanaout...
Read More
Unapotokwa na damu puani fanya yafuatayo;
1. Simama wima na inamisha kichwa kwa mbele, kusim...
Read More
Kuchagua vyakula sahihi kwa mlo wako inaweza kuwa changamoto na tungependa kuamini kwamba kupungua u...
Read More
Juisi hii ni nzuri sana katika kutibu shinikizo la juu la damu.
Lakini inaweza pia kutumika...
Read More
No comments yet. Be the first to share your thoughts!