Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/personal/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁
AckyShine

Ushauri kwa vijana wenye miaka 22 nakuendelea

Featured Image

Ikiwa wewe ni kijana na Una umri wa kuanzia miaka 22 na Kuendelea
Soma hapa ujifunze maisha ya hekima na namna bora ya kuishi na kufanikiwa ungali kijana

1. Kama uko shule au chuo soma na usicheze ukifeli unajipotezea muda. Soma sana utafanikiwa…

2. Jifunze kuweka akiba ya pesa. Pia jifunze kuwa na matumizi mazuri ya pesa,bajeti vizuri na jiwekee akiba bank au popte unapoona panafaa.

3. Jitengenezee good character yaani tabia yako njema ili uwe tofauti na wengine.. Jitofautishe na wengine, uwe mfano bora

4. Jifunze kufanya kazi tofauti tofauti. Fanya hiki ama kile ili angalau uweze kuishi popote kwani dunia inabadilikaa na huwezi jua kesho yako

5. Anza kununua na kumiliki vitu kama kitanda godoro vyombo na ardhi au kiwanja. Kumbuka msingi mzuri wa maisha ni fikra za ujana na kujiwekea mali

6. Kama utaweza kapange ujifunze maisha. Anza kujitegemea ili kujipa confidenece na maisha.

7. Weka falsafa yako katika maisha na uiishi. Falsafa ni dira ya kukuongoza. Mfano unataka kumiliki nini katika maisha? Unataka mke au mume wa aina gani? Aina gani ya maisha unaipenda? Hiyo ndiyo falsafa…

8. Tengeneza mahusiano yaliyotulia na weka malengo. (Kwa wale wa ndoa) Jichagulie kijana au binti aliyemzuri katika wengi, kijana au binti wa moyo wako, mpende… Kipindi hiki ni cha kuwa na mwenza aliyetulia kama unafikiri kuoa au kuolewa. Ukicheza ukafikisha 30 bila kuwa na mtu maaalumu basi utaoa au kuolewa bora mradi ila siyo na mtu wa ndoto yako..

9. Kuwa na marafiki imara, jichagulie katika wengi marafiki kadhaa waliotulia wenye nidhamu ya maisha na wanaopenda uende mbele. Kijana chunga marafiki ulionao wengi leo wanajuta kwaa urafiki m'baya uliowapoteza… a

10. Kumbuka ibada na kumshukuru Mungu. Kipindi hiki ni cha misukosuko na mihemko mingi. Usiache mafundisho ya imani yako, usimsahau Mungu. Mshukuru Mungu kwa uhai na kila jema au baya likupatalo.

11. Jitume katika kazi, watu waliofanikiwa wanajua thamani ya juhudi na kujituma. Usikate tamaa hata kama unapata kidogo. Fanya kazi kama vile kesho haipo. Matunda utayaona

12. Zingatia kujiweka safi. Kuwa msafi na mtanashati huanza na ubongo, muonekano wako ndivyo watu watakavyo kuchukulia. Jiweke safi na jitunze..

13. Kula kwa afya, wengi wanachukia miili yao. Wanauchukia aidha unene au wembamba, ila ukila kwa afya, ukafanya mazoezi unatengeneza afya bora ya sasa na baaadae..

14. Vaa kwa heshima, usivae kama mcheza disko au teja. Kumbuka thamani yako kwa Mungu. Kwanini uvae nguo za machukizo mbele yake! Kwanini ukubali kuwa wakala na kutumiwa na shetani kuwaaangamiza wengine kwa kuvaa ovyo? Vaa kwa heshima..

15. Pendelea kusafiri maeneo tofauti na ujifunze! Asafiriye hupata maarifa na hujifunza mengi. Penda kusafiri, tembelea maeneo tofauti utakuwa na mengi ya kujifunza.

16. Kumbuka kupumzisha mwili. Kuishi kwetu kupo katika chembe ya uhai iliyopo mwilini. Upe mwili na ubongo chakula chake cha kupumzika. Nenda maeneo yatakayofanya mwili na akili vipumzike angalau kila baada ya miezi kadhaa..

17. Jifunze kuamua mwenyewe. Usisubiri kila kitu kumshirikisha mtu ndio uamue. Jifunze kuwa mwamuzi wa mambo yako mwenyewe haijalishi kwa gharama ipi. Watu wawe washauri ila ubaki kuwa mwamuzi mwenyewe.

18. Kuwa mtu wa kutunza siri. Jitahidi kuwa na shingo nzito na akili yenye kuweka siri. Usiwe mtu wa kusema kila uonacho au uambiwacho.

19. Jfunze na zitawale hisia zako. Hisia ziwe za hasira, mapenzi au ugomovi zitawale na utaishi miaka mingi. Asiye tawala hisia zake hata awe mkubwa bado ni mdogo…

20. Jitolee kwaajili ya wengine, fundisha kemea saidia. Unaweza kufundisha kupitia facebook wasap nk. Kemea ukiona mtu anafanya kitu kibaya, saidia wenye shida wakumbuke wagonjwa yatima wazee na wenye mahitaji. Wewe ni yatima, mzee, au muhitaji wa kesho.. Weka akiba ya wema

21 Jenga mazingira ya kuishi na watu vizuri. Usijione mzuri au HB sana ukadharau wengine. Ishi na kila mtu kwa upendo hata kama wanakuchukia..

22. Tunza muda, muda ni mali huwezi kuurudisha, kuusimamisha au kuuzuia. Ukishapotea ndio basi tena. Tambua thamani ya muda na fanya vitu kwa wakati..

23. Pendelea kusoma hasa vitabu vya dini, kuhusu mali, elimu, mchumba, afya, maisha, uongozi, hekima, busara, utu, uchaji, utii, maarifa, utajiri, heshima, uvumilivu, matumaini, upendo, na kila kitu vimo katika Biblia na Qur'an ..soma uchote hekimaa…

24. Acha kujifunza matumizi ya pombe, sigara , dawa za kulevya. Kama unatumia jitahidi uache, kama unajifunza acha na kama kuna mtu anakushawishi kataa. Afya ni mali na mtaji usichoshe na kuumiza uhai wako kwa pombe sigara na madawa ya kulevya…

Inafaa ukishare kwa wengine wajifunze maarifa haya..
*Maisha ni maamuzi yako wewe*
Kuamua kufanikiwa au kushindwa,
kuamua utajiri au umasikini yote ni mipango na hutokana na fikra zako..

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Kuhamasisha Ushirikiano wa Kujenga na Kuunga Mkono Malengo ya Kila Mwanafamilia

Kuhamasisha Ushirikiano wa Kujenga na Kuunga Mkono Malengo ya Kila Mwanafamilia

Kuhamasisha Ushirikiano wa Kujenga na Kuunga Mkono Malengo ya Kila Mwanafamilia

Familia ni... Read More

Mbinu 6 za Kujenga Uhusiano wa Kimwili na Kihisia na mke wako

Mbinu 6 za Kujenga Uhusiano wa Kimwili na Kihisia na mke wako

Kujenga uhusiano wa kimwili na kihisia na mke wako ni muhimu katika kuimarisha ndoa na kuendeleza in... Read More
Namna ya Kujenga Mazoea ya Shukrani na Furaha na mke wako

Namna ya Kujenga Mazoea ya Shukrani na Furaha na mke wako

Kujenga mazoea ya shukrani na furaha na mke wako ni muhimu sana katika kuimarisha uhusiano wenu. Hap... Read More
Jinsi ya Kuelewa na kukabiliana na mabadiliko ya kijamii na kitamaduni na mpenzi wako

Jinsi ya Kuelewa na kukabiliana na mabadiliko ya kijamii na kitamaduni na mpenzi wako

Mabadiliko ya kijamii na kitamaduni huwa ni sehemu ya maisha yetu, na kwa wakati mwingine yanawez... Read More

Kukabiliana na Mazoea ya Kutokujali katika Mahusiano: Kuweka Thamani na Heshima

Kukabiliana na Mazoea ya Kutokujali katika Mahusiano: Kuweka Thamani na Heshima

Mahusiano ni muhimu sana katika maisha yetu ya kila siku. Lakini katika mahusiano, mara nyingi tu... Read More

Kusisimua Mwili na Akili: Jinsi ya Kuleta Msisimko katika Kufanya Mapenzi

Kusisimua Mwili na Akili: Jinsi ya Kuleta Msisimko katika Kufanya Mapenzi

Kusisimua Mwili na Akili: Jinsi ya Kuleta Msisimko katika Kufanya Mapenzi

Mapenzi ni moja ... Read More

Jinsi ya Kuwa Wazazi Wanaoongoza na Kuhamasisha Watoto: Sifa na Mbinu

Jinsi ya Kuwa Wazazi Wanaoongoza na Kuhamasisha Watoto: Sifa na Mbinu

Karibu kwenye makala hii inayokusaidia kuwa mzazi mwenye uongozi na uhamasishaji kwa watoto wako.... Read More

Jinsi ya Kufanya Familia kuwa Kitovu cha Huduma na Kujitolea: Kuleta Mabadiliko Chanya

Jinsi ya Kufanya Familia kuwa Kitovu cha Huduma na Kujitolea: Kuleta Mabadiliko Chanya

  1. Kuanzisha mazungumzo ya familia: Familia inapaswa kuwa kitovu cha huduma na kujitolea. ... Read More

Mbinu za Kupata Tarehe na Wasichana kwa Mafanikio

Mbinu za Kupata Tarehe na Wasichana kwa Mafanikio

Leo, tunazungumzia mbinu za kupata tarehe na wasichana kwa mafanikio. Kila mtu anataka kuwa na mp... Read More

Kuishi na Tofauti za Kijinsia: Kuelewa na Kuheshimu Uwepo wetu Wote

Kuishi na Tofauti za Kijinsia: Kuelewa na Kuheshimu Uwepo wetu Wote

Kuishi na Tofauti za Kijinsia: Kuelewa na Kuheshimu Uwepo wetu Wote

Leo hii, dunia ina ida... Read More

Njia za Kukabiliana na Kukosa Hamu ya Kufanya Mapenzi: Kurejesha Nguvu ya Mapenzi

Njia za Kukabiliana na Kukosa Hamu ya Kufanya Mapenzi: Kurejesha Nguvu ya Mapenzi

Kukosekana kwa hamu ya kufanya mapenzi ni tatizo ambalo huathiri watu wengi, haswa wapenzi. Tatiz... Read More

Jinsi ya Kuwa na Mazungumzo ya Mafanikio na Watoto: Kukuza Uwezeshaji na Kujiamini

Jinsi ya Kuwa na Mazungumzo ya Mafanikio na Watoto: Kukuza Uwezeshaji na Kujiamini

Leo hii tutazungumzia kuhusu jinsi ya kuwa na mazungumzo ya mafanikio na watoto. Kuwa na mazungum... Read More

📖 Explore More Articles
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About