Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/personal/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ
AckyShine

Ushauri wa ukweli Ili Uwe mwanaume wa Ukweli

Featured Image

1. Ukija kijiweni au pub au kwenye nyama choma acha zile stori za sijui umesoma wapi hadi wapi, sijui una madigirii mangapi. Piga stori nyingine, mbona ziko nyingi tu. Kujielezea sana shule yako ni ushamba fulani hivi, dizaini kama hujiamini so lazima ujivishe nyota. Unaboa.

2. Tembea na keshi mfukoni kama vipi, stori za kadi yangu ya benki imegoma sio ishu.

3. Punguza mambo yako ya kuvaa sana kipapaa. Sometimes ibuka na pensi na jinsi tu mwana.

4. Punguza kukesha nje mfululizo, iwe umeoa, una mpenzi au upo upo. Kikanuni kabisa usikae nje hadi usiku wa manane siku tatu mfululizo labda uwepo mchongo wa maana sana. I mean wa maana sana.

5. Epuka sana mchezo wa kujipiga tattoos. Kuna watu wamekosa wake au michongo hevi in life kisa hizo mambo.

6. Nasisitiza sana epuka kumtaka mpenzi wa zamani wa mshikaji wako. Pigia mstari hii pointi. Kwani lazima upite palepale? Tusiishi kikondoo bro.

7. Jiunge walau na mtandao mmoja wa kijamii. Keep in touch na washikaji. Kuna wana toka mmemaliza primary hamjachekiana, utawakuta mitandaoni. Unaweza kupata mchongo au kujifunza ishu mbili tatu, au kuwa fala zaidi ukiamua.

8. Maisha mafupi sana, jitahidi kupunguza kukunja ndita. Jiachie mara moja moja.

9. Ukifika baa uwe tayari unajua unakunywa nini. Sio Mhudumu anakuja kukusikiliza unawaaaaaza. Inaonyesha hujisomi na huna mipango. Samahani lakini.

10. Kama hujaalikwa kwenye ishu, usiende mwanangu. Sometimes hata ukialikwa usiende pia. Unaweza kualikwa ili useme no, kiushahidi tu.

11. Halafu tumechoka wewe kuwa kituko ukilewa. Kama pombe huziwezi ziache, piga juisi tu au maji wakati wana tunapiga monde, sio kesi, ni uwezo tu wa kuhimili.

12. Toa tip bila kuomba namba ya baamedi basi mwanangu. Jifanye kama umetoa tu msaada. Hata simba sio swala wote huwa anawala porini, wengine anawacheki anapita zake.

13. Punguza kutumia simu sana, tena wakati mwingine kwa ishu ambazo hazina mpango.
Ukumbuke juzi juzi hapa wataalamu wamesema simu zinaleta ugumba.

14. Nunua tumiwani twa jua twa bei bei hivi, inakupa mwonekano wa kijentlomani sometimes.

15. Piga push-ups walau 50, sit ups na dips kabla ya kuoga asubuhi, hii afya tumeazimwa tu, jiweke fit.

16. Toka out na washikaji zako at least mara moja kwa mwezi mpige msosi na kinywaji. Wife au demu wako na wanao waache home! Sio kila kona kila siku uko nao kama mkoba, kichwa kitatia kutu.

17. Julikana walau hata baa mbili tatu au sehemu mbili tatu. Baa, basketball ground, soccer ground, acha kujikunyata home. Wewe mtoto wa kiume man.

18. Jifanye mjuaji sometimes, then jifunze baadaye. Sio kila kitu wewe ni โ€œI donโ€™t knowโ€.

19. Beer moja au glass moja ya wine baada ya mlo haiwezi kukuvurga, kama hutaki, kunywa majuisi yako basi ulete inzi, au misoda ujijazie magonjwa.

20. MTOTO WA KIUME HAPIGI SELFIE OVYO OVYO NA KUBINUA MIDOMO na KULAMBA LIPSI. PIGA SELFIE KWENYE ISHU MUHIMU. FAMILIA HIVI, DEMU MKALI, etc. Umenisoma?

21. Ukiweza miliki hata panga ghetto, maana bastola najua ngumu. Sio nyumba nzima huna hata kasilaha kadogo.

22. Ridhika. Hamna hata siku moja utakuwa na kila kitu. Jifunze kushukuru kwa ulicho nacho.

23. Sometimes agiza matunda badala ya chipsi.

24. Ukikutana na demu mzuri kiwanja yuko peke yake, muongeleshe.

25. Miliki walau suti moja kabla hujapitisha miaka 30 bro. Please. Na tupafyumu.

26. Kuwa na mpenzi moja
kwa wakati mmoja. Anatosha sana. Trust me.

27. Ukitaka kujilinganisha, jilinganishe wewe wa jana na wewe wa leo. Utafika mbali. Ukijilinganisha na wana utapasuka kichwa.

28. Piga picha nyingi kwa camera (again, sio selfies) tunza kumbukumbu.

29. Ukialikwa kwenye party usiende mikono mitupu. Nenda walau na kachupa kamoja ka mvinyo.

30. Date demu nje ya wale unaokutana nao club au baa mara wa mara. Utakuja kuniambia faida zake.

31. Huwezi kuwa mpenzi wa pombe au sigara kwa sababu hivyo vitu havitakaa vikupende.

32. Hata siku moja usirudiane na demu aliyekuacha kisa huna mkwanja. Kaenda kutafuta kakosa ndio maana kakurudia labda baada ya kuona umepata. Siku akikutana na mwenye chambi kukuzidi? Jibu kaa nalo.

33. Sometimes jitoe out mwenyewe, kaa mahali piga msosi wako na kinywaji chako, tafakari ishu zako. Alone.

34. Jisomee ukiwa na time. Inakupa chance kuazima ubongo wa mtu mwingine lakini pia inakupa matirio kwenye maongezi, ila stori za kuja kwenye joint na washikaji na kuanza kusema oh nimesoma kitabu hiki na kile kausha!

35. Puuza wanaozomea. Huwa wamekaa viti vile vya bei rahisi.

36. Hata siku moja usiseme โ€œNdo hivyo bwana, hamna namna tenaโ€. Ipo namna bro.

37. Usi-bet kama ukipoteza buku 5 we ni mtu wa kulia lia kindezi.

38. Muombe na Mshukuru Mungu wako. Kama huna Mungu jishukuru mwenyewe, kiazi wewe.

39. Kumbuka, sheria hufuatwa na wajinga lakini huwaongoza wenye busara.

Kama Mwanamme Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE
[products columns="2" ids="30827"]
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Kujenga Mazingira ya Upendo na Kujali katika Familia Yako

Kujenga Mazingira ya Upendo na Kujali katika Familia Yako

Familia ni moja ya mazingira muhimu kuliko yote katika maisha yetu. Ni mahali ambapo tunakulia, t... Read More

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu uzazi na mipango ya familia

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu uzazi na mipango ya familia

Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu uzazi na mipango ya familia ni mchakato muhimu katika uhusiano wen... Read More
Jinsi ya Kuelewa na kuheshimu mafanikio na changamoto za kazi za mpenzi wako

Jinsi ya Kuelewa na kuheshimu mafanikio na changamoto za kazi za mpenzi wako

Kama mpenzi wako ana kazi, ni muhimu kuelewa na kuheshimu mafanikio na changamoto zake. Hii itaon... Read More

Kuimarisha Ushawishi wa Mwenzi katika Kufanya Mapenzi: Kuelewa na Kujibu Mahitaji yao

Kuimarisha Ushawishi wa Mwenzi katika Kufanya Mapenzi: Kuelewa na Kujibu Mahitaji yao

Mapenzi ni sehemu muhimu sana katika maisha yetu, na kila mtu anapenda kufanya mapenzi yenye ubor... Read More

Kuboresha Mawasiliano ya Kijinsia katika Uhusiano wa Kufanya Mapenzi

Kuboresha Mawasiliano ya Kijinsia katika Uhusiano wa Kufanya Mapenzi

Habari wapenzi! Leo tutaongelea suala zito kuhusu kuboresha mawasiliano ya kijinsia katika uhusia... Read More

Kuimarisha Mazungumzo ya Uaminifu na Heshima katika Mahusiano

Kuimarisha Mazungumzo ya Uaminifu na Heshima katika Mahusiano

Mahusiano yoyote yana uzoefu wa changamoto, lakini kuwa na mazungumzo ya uaminifu na heshima ndiy... Read More

Kukabiliana na Changamoto za Kufanya Mapenzi katika Uhusiano

Kukabiliana na Changamoto za Kufanya Mapenzi katika Uhusiano

Kukabiliana na Changamoto za Kufanya Mapenzi katika Uhusiano

Katika uhusiano wowote wa kim... Read More

Ushawishi wa Vyombo vya Habari katika Maoni yetu ya Kufanya Mapenzi: Kuchambua na Kuelimisha

Ushawishi wa Vyombo vya Habari katika Maoni yetu ya Kufanya Mapenzi: Kuchambua na Kuelimisha

Ushawishi wa vyombo vya habari katika maoni yetu ya kufanya mapenzi ni suala ambalo limekuwa liki... Read More

Jinsi ya Kusaidiana na Kuunga Mkono katika Familia: Nguvu ya Ushirikiano

Jinsi ya Kusaidiana na Kuunga Mkono katika Familia: Nguvu ya Ushirikiano

Familia ni kitu muhimu sana katika maisha yetu. Inatupa nguvu, faraja, na upendo. Hata hivyo, kun... Read More

Jinsi ya Kuwa na Mazungumzo ya Kufurahisha na Watoto: Kujenga Kumbukumbu za Kucheka

Jinsi ya Kuwa na Mazungumzo ya Kufurahisha na Watoto: Kujenga Kumbukumbu za Kucheka

Leo hii, nataka kuzungumzia jinsi ya kuwa na mazungumzo ya kufurahisha na watoto. Ni muhimu sana ... Read More

Jinsi ya Kuelewa na kukabiliana na changamoto za kusaidia na kuwajali watu wenye matatizo ya kiafya ya akili

Jinsi ya Kuelewa na kukabiliana na changamoto za kusaidia na kuwajali watu wenye matatizo ya kiafya ya akili

Watu wengi huwa na matatizo ya kiafya ya akili na hukabiliana na changamoto nyingi za kila siku. ... Read More

Kujenga Ushirikiano wa Karibu na Wazazi na Familia katika Mahusiano

Kujenga Ushirikiano wa Karibu na Wazazi na Familia katika Mahusiano

  1. Kuwa wazi na Wazazi na Familia Kujenga ushirikiano wa karibu na wazazi na familia ni mu... Read More

๐Ÿ“– Explore More Articles
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About