Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/personal/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Kwa nini wasichana wakiingia utu uzima damu zinaanza kutoka kwenye uke?

Featured Image
Kutoka damu (hedhi) kwa mara ya kwanza kunaitwa kuvunja ungo na hii ni dalili ya mtoto wa kike kuingia utu uzima,0 yaani kuwa mwanamke. Wasichana wanavunja ungo kati ya umri wa miaka 8 na umri wa miaka 18. Lakini, kuvunja ungo haina maana kwamba unahitaji kuanza kujamii ana. Kwa sababu ukijamii ana kuna hatari ya kupata mimba! Mwanzoni siku za hedhi zinaweza kuwa na mabadiliko sana. Ni baada ya muda ndipo msichana anaanza kwenda mwezini mara moja kila mwezi. Kwa wanawake wengi ni kila baada ya siku 28, hata hivyo, wengine huweza kupata hedhi chini au zaidi ya siku hizo. Idadi ya siku katika mzunguko wa hedhi ni siku 21 hadi 35.Ukitaka kuelewa kabisa maana ya kutoka damu za mwezi, lazima nieleze kuhusu mzunguko wa hedhi. Siku ya kwanza ya damu huhesabiwa kama siku ya kwanza ya mzunguko. Baada ya damu kutoka, yai moja linaanza kukua ndani ya kokwa. Na vilevile utando ndani ya mfuko wa uzazi huanza kujengeka ili ukaribishe mimba. Kati ya siku 11 au 14 yai hupevuka ndani ya kokwa na halafu husafiri kwenye mirija ya kupitishia mayai hadi kwenye mfuko wa uzazi. Mwanamke anapata mimba kama yai likirutubishwa na mbegu ya kiume ndani ya mirija ya kupitisha mayai, i ina maana, kwamba atakuwa amejamii ana kipindi cha siku chache kabla ya yai kupevuka au siku yai linapopevuka. Kama yai halikurutubishwa, basi hufa na hutangulia kutoka kama ute, pia utando kwenye mfuko wa uzazi na kuta za uzazi hubomoka na kutoka kama damu. Hii ndiyo hedhi yenyewe. Endapo msichana amejamiiana na mvulana na yai likarutubushwa, hataona hedhi na aelewe kwamba kuna uwezekano kwamba mimba imetungwa. Mzunguko wa hedhi kwa baadhi ya wasichana hauna mpangilio mwanzoni, hivyo endapo hupati hedhi inayolingana kila mwezi usijali. Katika hali ya kawaida usipopata hedhi na hukujamiiana na mvulana, basi inawezekana ni mabadiliko tu ya mwili. Hali hii ikiendelea au ukiwa na wasiwasi unashauriwa kumuona mtaalamu wa afya
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Je, kuna madhara msichana akifanya mapenzi wakati akiwa katika hedhi (siku zake)?

Je, kuna madhara msichana akifanya mapenzi wakati akiwa katika hedhi (siku zake)?

Kufanya mapenzi wakati msichana yuko katika hedhi hakuna madhara yoyote kiafya kwa mwanaume wala ... Read More

Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano Mazuri ya Simu na Msichana

Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano Mazuri ya Simu na Msichana

Kama una nia ya kuimarisha uhusiano wako na msichana, ni muhimu kuwa na mawasiliano mazuri ya sim... Read More

Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano Mzuri na Msichana

Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano Mzuri na Msichana

Leo tutazungumzia jinsi ya kuwa na mawasiliano mzuri na msichana. Kwa sababu ya tofauti za kijins... Read More

Je, ninaweza kuambukizwa na Virusi vya UKIMWI na UKIMWI kwa kuumwa na mbu?

Je, ninaweza kuambukizwa na Virusi vya UKIMWI na UKIMWI kwa kuumwa na mbu?

Hapana, mbu na wadudu wengine hawawezi i kukuambukiza virusi vya UKIMWI kutokana na mfumo wa mii ... Read More

Je, nikila na mtu mwenye Virusi vya UKIMWI, nitaambukizwa na virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Je, nikila na mtu mwenye Virusi vya UKIMWI, nitaambukizwa na virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Hapana, ukila na mtu mwenyemaambukizi ya Virusi vya UKIMWI huwezi kuambukizwa Virusi vya UKIMWI w... Read More

Je, ngono/kufanya mapenzi ni sehemu muhimu ya uhusiano wa kimapenzi?

Je, ngono/kufanya mapenzi ni sehemu muhimu ya uhusiano wa kimapenzi?

Je, ngono/kufanya mapenzi ni sehemu muhimu ya uhusiano wa kimapenzi?

Kwa wengi, kufanya ma... Read More

Unyanyasaji wa kijinsia

Unyanyasaji wa kijinsia

Kuna aina nyingi za unyanyasaji wa jinsia na unaweza kutokea kwa wote wanaume na wanawake. Kwa kawai... Read More
Inakuwaje mtoto anakuwa wa kike au wa kiume?

Inakuwaje mtoto anakuwa wa kike au wa kiume?

Mwili wa mwanaume unatengeneza aina mbili za mbegu. Kuna mbegu zinazokua kuwa mtoto wa kiume na k... Read More

Jinsi ya kutumia Kondomu

Jinsi ya kutumia Kondomu

Wakati wa kutumia kondomu ya kiume ni muhimu kufuata hatua zifuatazo. Hakikisha kwamba pakiti ina... Read More

Je, watu wanapendelea kujaribu njia za kuleta msisimko wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wanapendelea kujaribu njia za kuleta msisimko wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Karibu sana kwenye makala hii ya blog, ambapo tutajadili kuhusu kwa nini watu wanapendelea kutafu... Read More

Je, kuna tofauti za umri katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna tofauti za umri katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna tofauti za umri katika ngono/kufanya mapenzi? Ndio, kuna tofauti nyingi sana! Hiyo ndiyo... Read More

Madhara yatokanayo na ukeketaji

Madhara yatokanayo na ukeketaji

Ukeketaji au tohara ya wanawake ni hatari sana kwa msichana anayetahiriwa. Wasichana hufa kutokana n... Read More
πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About