Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/personal/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Madhara ya dawa za kulevya kwa mwili na ubongo

Featured Image
Moja kati ya vitu vinavyotisha kuhusu dawa za kulevya ni kwamba zinaathiri watu kwa njia mbalimbali na huwezi ukasema kwa uhakika jinsi zitakavyokuathiri. Madhara ya dawa za kulevya yanategemea aina, kiwango na jinsi zitakavyotumika. Vilevile inategemea na umri, afya ya mwili na ukomavu wa akili, na pia mazoea ya matumizi ya dawa hizo. Madhara ya muda hutokea mara tu baada ya dawa za kulevya kutumika, wakati madhara ya muda mrefu huonekana baada ya muda kupita, na mara nyingi husababisha uharibifu wa kudumu kwenye mapafu na ubongo. Kwa mfano, bangi, husababisha kuongezeka kwa mapigo ya moyo, matatizo ya kumbukumbu ya muda mfupi, pamoja na umakini, kujifunza, kufikiri na kutatua matatizo. Pia inaweza ikasababisha kasoro kwenye utaratibu wa viungo vya mwili. Mara kwa mara wavuta bangi huwa na macho mekundu. Na vijana wengine hupata mihemuko mbalimbali kama uoga na hofu baada ya matumizi ya bangi. Dawa za kulevya za vichangamsho, kama mirungi na kokaini, inasemekana kuwa huwafanya watumiaji kuwa macho, kujiona wana nguvu na kujiamini. Vichangamsho vikitumika kwa wingi, humfanya mtumaji kujihisi kuwa na wasiwasi au hofu. Matumizi mabaya ya dawa za kulevya kwa muda mrefu huweza kusababisha matatizo ya akili au hata kifo i iwapo yatatumika kwa kiwango cha juu. Dawa za kulevya zinazokufanya upooze kama heroini au dawa nyingine zinazoagizwa na daktari, husababisha kujisikia umetulia, una amani na furaha. Ukizidisha vipimo husababisha usingizi, upungufu wa umakini na uwezo wa kuona, kizunguzungu, kutapika na kutokwa jasho. Vilevile kipimo kingi kinaweza kusababisha usingizi wa muda mrefu, kuzimia na hata kifo. Pombe za kienyeji kama gongo ni hatari kwa afya na zinaweza kusababisha upofu na hata kifo. Matumizi ya dawa za kulevya hupunguza uwezo wa vijana kuhimili na kutatua matatizo yao ya kijamii na kiakili. Hii husababisha vijana kuwa wepesi kujihusisha na ujambazi na mambo ya ngono na ugomvi, mabadiliko hayo ya tabia husababisha ugomvi katika familia na kuvunjika kwa urafiki. Matumizi ya dawa za kulevya ndiyo sababu kubwa ya ajali za barabarani, kujiua na maambukizo mbalimbali.
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Je, kuna umuhimu wa kuelewa na kuheshimu mipaka ya kisaikolojia katika uhusiano wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu wa kuelewa na kuheshimu mipaka ya kisaikolojia katika uhusiano wa ngono/kufanya mapenzi?

Kuelewa na kuheshimu mipaka ya kisaikolojia katika uhusiano wa ngono/kufanya mapenzi ni muhimu sa... Read More

Ubikira ni nini?

Ubikira ni nini?

Maana halisi ya neno β€œbikira” ni mwanamke au mwanaume ambaye hajawahi kabisa kujamii ana. Kuj... Read More

Jinsi ya Kusimamia Uchungu wa Kupendwa na Msichana

Jinsi ya Kusimamia Uchungu wa Kupendwa na Msichana

Jinsi ya Kusimamia Uchungu wa Kupendwa na Msichana

Kupendwa na msichana ni jambo la kufura... Read More

Je, ni kweli kuwa ulemavu unaweza kugundulika mara tu mtoto anapozaliwa?

Je, ni kweli kuwa ulemavu unaweza kugundulika mara tu mtoto anapozaliwa?

Ni kweli kuwa daktari anaweza kufanya vipimo vya kugundua
kama mtoto aliye tumboni ni mwenye... Read More

Kujikinga na Maambukizi ya UKIMWI: Njia za Kuepuka Hatari

Kujikinga na Maambukizi ya UKIMWI: Njia za Kuepuka Hatari

Kujikinga na Maambukizi ya UKIMWI: Njia za Kuepuka Hatari

  1. Jambo zuri ni kuwa na ... Read More

Je, kuna umuhimu wa kujadili matakwa na matarajio yako ya ngono/kufanya mapenzi na mwenza wako?

Je, kuna umuhimu wa kujadili matakwa na matarajio yako ya ngono/kufanya mapenzi na mwenza wako?

Kama wapenzi, kujadili matakwa na matarajio yako ya ngono/kufanya mapenzi na mwenza wako ni jambo... Read More

Jinsi ya Kuwa na Siku ya Kumbukumbu ya Kipekee na Msichana

Jinsi ya Kuwa na Siku ya Kumbukumbu ya Kipekee na Msichana

Kumbukumbu zetu ni muhimu sana katika maisha yetu. Siku ya kumbukumbu ni siku muhimu sana kwa sab... Read More

Ni dawa zipi zilizopigwa marufuku Tanzania na nini hutokea pale mwingizaji anapokamatwa?

Ni dawa zipi zilizopigwa marufuku Tanzania na nini hutokea pale mwingizaji anapokamatwa?

Hapa Tanzania matumizi, umilikaji, usafirishaji na kuhusika katika dawa za kulevya kama vile bang... Read More

Jinsi ya Kujifunza Kutambua na Kuheshimu Makubaliano ya Kufanya Ngono

Jinsi ya Kujifunza Kutambua na Kuheshimu Makubaliano ya Kufanya Ngono

Jinsi ya Kujifunza Kutambua na Kuheshimu Makubaliano ya Kufanya Ngono 🌝

Karibu vijana w... Read More

Kwa nini Albino wanawekwa katika kundi la watu wenye ulemavu?

Kwa nini Albino wanawekwa katika kundi la watu wenye ulemavu?

Ulemavu maana yake ni hitilafu katika mwili au akili inayomwekea
mipaka mtu asiweze kufaniki... Read More

Jinsi ya Kuonyesha Utambulisho Wako kwa Msichana

Jinsi ya Kuonyesha Utambulisho Wako kwa Msichana

Jinsi ya Kuonyesha Utambulisho Wako kwa Msichana

Kuonyesha utambulisho wako kwa msichana n... Read More

Je, kuwa kuna mambo ambayo hayafai kuzungumziwa kuhusu ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuwa kuna mambo ambayo hayafai kuzungumziwa kuhusu ngono/kufanya mapenzi?

Habari yako, mpenzi! Katika mada ya leo, tunajadili kuhusu mambo ambayo hayafai kuzungumziwa kuhu... Read More

πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About