Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-25 10:23:14 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Ndizi - 15 takriiban
Nayma ya ng’ombe - 1 kilo
Kitunguu maji - 1
Nyanya - 3
Kitunguu saumu(thomu/galic) kilosagwa - 1 kijiko cha supu
Tangawizi mbichi ilosagwa - 1 kijiko cha supu
Pilipili mbichi ilopondwa - 2
Jira/cummin/bizari ya pilau ilosagwa - 1 kijiko cha chai
Ndimu - 1
Chumvi - kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Chemsha nyama kwa ndimu, chumvi na tangawizi mbichi na kitunguu thomu. Menya ndizi na zikatekate vipande kiasi, weka katika sufuria. Katakata kitunguu na nyanya utie katika ndizi. Tia jira na chumvi. Nyama ikiwiva mimina pamoja na supu yake ufunike ndizi ziwive na kuwa tayari kuliwa. Ukipenda tia pilipili mbuzi zichemke pamoja na ndizi.
Updated at: 2024-05-25 10:34:41 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga - 3 Vikombe vya chai
Siagi - 250 gms
Baking powder - 3 Vijiko vya chai
Mayai - 2
Chumvi - 1 kijiko cha chai
Maziwa - 1/2 Kikombe
Pilipili manga ya unga 1 Kijiko cha chai
MAANDALIZI
Katika bakuli la kusagia (blender) au mashine ya keki, tia siagi, chumvi na mayai, piga mpaka iwe kama malai (cream). Tia Unga, baking powder, pilipili manga. Tia maziwa. Kata usanifu (design) unayotaka na sokota au kunja kwa usanifu unaopenda. Pika (bake) katika moto wa 350º C – usiviache vikawa rangu ya udongo (brown) sana.
Mapishi ya Pilau Ya Adesi Za Brown Karoti Na Mchicha Kwa Samaki Wa Salmon
Updated at: 2024-05-25 10:37:37 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Mchele vikombe 3
Karoti 1 ikune (grate)
Mchicha katakata kiasi
Adesi za brown
Kitunguu katakata (chopped)
Supu ya kitoweo chochote upendayo au vidonge vya supu 2
Garama masala (bizari mchanganyiko) kijiko 1 cha kulia
Samli ¼ kikombe
Chumvi kiasi
Vipimo Vya Samaki Wa Salmon
Samaki wa Salmon vipande 4 vikubwa
Tangawizi mbichi ilosagwa kijiko 1 cha kulia
Thomu (garlic/saumu) kijiko 1 cha kulia
Chumvi kiasi
Bizari ya mchuzi kijiko 1 cha kulia
Ndimu 1 kamua
Nyanya 2 kata slice kubwa kubwa
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Samaki wa Salmon
Changanya viungo vyote upake katika samaki. Weka katika treya na panga slice za nyanya juu yake. Oka (grill/choma) katika oven umgeuze samaki upande wa pili. Akiwa tayari epua.
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Wali
Roweka mchele kiasi kutegemea aina ya mchele. Tumia basmati (pishori) Roweka adesi kisha zichemshe katika maji ya kiasi. Chuja maji adesi na maji yatakayobakia tumia katika kupikia pilau hii. Kaanga vitunguu katika samli iliyoshika moto kwenye sufuria ya kupikia. Vikianza kugeuka rangi tia karoti, mchicha, adesi, bizari mchanganyiko kisha kaanga kidogo. Tia mchele ukaange kidogo kisha tia supu au maji pamoja na kidonge cha supu. Tia chumvi ukoroge funika upike kama pilau. Epua upakue katika sahani utolee kwa samaki wa salmon
Updated at: 2024-05-25 10:23:06 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga - 4 Vikombe vya chai
Siagi - 1 Kikombe cha chai
Hiliki ½ Kijiko cha chai
VIAMBAUPISHI:SHIRA
Sukari - 2 Vikombe vya chai
Maji - 1 Kikombe cha chai
Vanilla ½ Kijiko cha chai
(cocoa ukipenda kugawa visheti aina mbili) 2 Vijiko vya chai.
JINSI YA KUTENGENEZA
Tia unga kwenye bakuli pamoja na siagi na hiliki. Changanya vizuri isiwe na madonge. Tia maji baridi vikombe viwili kasoro vya chai changanya ukiona bado ongeza maji kidogo, iwe kama chapati usikande uchanganye tu. Halafu utakata sampuli unayopenda mwenyewe. Unaweka karai ya mafuta yakisha kupata moto unaanza kuchoma moto usiwe mkali sana, kiasi, baadae unaweza kuongeza moto na vikaange hadi viwe rangi ya dhahabu, kisha viepue vichuje mafuta. . Ukipenda gawa visheti sehemu mbili, na shira pia igawe sehemu mbili Changanya nusu ya visheti kwa shira nyeupe. Nusu ya shira nyingine ibandike tena motoni na tia cocoa vijiko viwili vidogo vya chai. Inapochanganyika cocoa vizuri changanya nusu ya visheti ulivyogawa kupata visheti vya shira ya cocoa.