Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-25 10:35:10 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kuchagua vyakula sahihi kwa mlo wako inaweza kuwa changamoto na tungependa kuamini kwamba kupungua uzito ni jambo tu la kula kalori chache na kufanya mazoezi zaidi. Hata hivyo, si mara zote zoezi hili linakuwa rahisi. Kama ni lengo lako kupunguza uzito, kuchagua chakula gani ule ni muhimu kama kuchagua kiasi gani cha chakula ule.
Ukweli ni kwamba , baadhi ya vyakula vinauwezo wakusaidia kupunguza uzito kutokana na tabia zake za kuunguza mafuta mwilini.
Mafuta ya nazi yanapanda chati kwa haraka kabisa na kufanya kuwa mojawapo ya vyakula bora kabisa kwa afya ya binadamu.
Mojawapo ya vitu muhimu kabisa katika mafuta haya ni uwezo wake wa kupunguza uzito wa mwili.
Mafuta ya nazi ni yana kemikali yenye mlolongo wa kati wa mafuta (“Medium Fatty Chain Acids”) ambayo humeng’enywa tofauti na yale yenye mlolongo mrefu wa mafuta (“Long Fatty Chain Acids”)
Kemikali zenye mlolongo mrefu wa mafuta(“Long Fatty Chain Acids”) hupatikana kwa wingi katika vyakula vingi vya mafuta kaa vile nyama, chips n.k.
Kemikali zenye mlolongo wa kati wa mafuta hutumiwa na mwili kwa ajili ya nishati badala ya kuhifadhiwa kama mafuta katika mwili.
Hii ndio sababu mafuta ya nazi ni moja ya vyakula vyenye uwezo wa kuchoma mafuta mwilini na kusaidia kupungua uzito.
Siki ya Apple (Apple Cider Vinegar)
Siki ya Apple ina kiwango kikubwa cha kemikali za amino (amino acids) ,kemikali za kumeng’enya chakula na madini na vitamini. Utafiti unaonyesha kwamba kutumia Siki ya Apple kabla ya kula vyakula vya wanga inasaidia kupunguza kupanda kwa insulin hivyo kusaidia kutopata hamu ya kula mara kwa mara.
Ndimu na Limao
Utafiti unaonyesha kuwa kiasi cha vitamini C mwilini kinahusiana na uzito wa mwili.
Watu wenye viwango vya kutosha wa vitamini C wana uwezo wa uwezo wa kuvunja asilimia 30 zaidi ya mafuta wakati wa mwili unapofanya shughuli za nguvu kama kazi za nyumbani,shambani na mazoezi kama kutembea, kuliko wale walio na kiwango cha chini cha vitamini C.
Kama una dhamira ya kupungua uzito, basi fikiria kuanza siku yako kwa kunywa glasi moja ya maji yenye ndimu au limao au anza kutumia siki(vinegar) kwenye kachumbali au saladi unapokula chakula.
Balungi
Balungi yana kiasi kidogo cha kalori , kiwango cha juu cha tindikali za kumeng’enya chakula na inaweza kukufanya usijisikie njaa kwa muda mrefu.
Watafiti wamegundua kwamba kula nusu ya balungi kabla ya mlo ni inachangia sana kupoteza uzito . Pia kula nusu tu ya balungi kabla ya mlo inaweza kusababisha kupungua kwa kiasi cha glucose-insulin katika muda wa masaa mawili tu.
Kama wewe unahitaji kupungua uzito zingatia kula vyakula vinavyo kata mafuta na ongeza vyakula hivi vilivyotajwa katika mlo wako.
Kwa mafanikio ya muda mrefu , kazania kula vyakula kamili (vyakula visivyo kobolewa au kusindikwa) na kufanya mazoezi ya mara kwa mara.
Updated at: 2024-05-25 10:35:11 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mchanganyiko wa mdalasini na asali unasaidia katika mambo ya aiana tofauti tofauti kama ifutavto:
Kuvu au fungus miguuni
Changanya kijiko kimoja cha asali, vijiko viwili vya mdalasini na upake kwenye sehemu zilizoathirika usiku kwa muda wa nusu saa, kisha safisha kwa sabuni na maji fufutende.
Maumivu ya jino
Changanya vijiko viwili vya asali na kijiko kimoja cha mdalasini na utumia kukupunguzia maumivu ya jino.
Mafua
Tumia kijiko kimoja cha asali iliyochanganywa na robo kijiko cha mdalasini, mchanganyiko huu husaidia kuondoa chafya na kuvimba kwa koo.
Tumbo kusokota
Asali imetambuliwa kwa kipindi kirefu kwamba ni dawa ifaayo kuondoa kadhia ya tumbo kuchafuka. Unachohitaji kufanya ni kuongeza kiasi kidogo cha mdalasini kwenye asali na uchanganye kisha uongeze maji kikombe kimoja na unywe mchanganyiko huu.
Ugonjwa wa viungo
Tumia mchanganyiko wa kijiko kimoja cha asali, vijiko viwili vya maji ya ufufutende na kijiko 1 cha mdalasini na upake kwenye sehemu zilizoathirika.
Kukatika kwa nywele
Changanya asali, mdalasini na mafuta ya mizeituni kisha upake mchanganyiko huo kichwani na uache kwa dakika 15 kabla ya kuosha nywele zako.
Updated at: 2024-05-25 10:35:29 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Zifutazo ni faida zitokanazo na ulaji wa tende;
1. Tende huongeza nguvu kutokana na kuwa na sukari ya asili, unaweza kuchanganya na maziwa na kupata mchanganyiko bora.
2. Tendehuzuia meno kuoza, na ni tiba nzuri kwa wagonjwa wa anemia kutokana na kuwa na madini mengi ya chuma.
3. Hupunguza uwezekano wa kupata Kiharusi (stroke) kwani hazina cholesterol kabisa! Pia zina vitamini na madini kwa wingi.
4. Hupunguza madhara ya pombe mwilini na kurudisha afya ya mtu.
5. Zina kiasi kikubwa cha kamba kamba ambazo hufanya mtu apate choo kirahisi na laini.
6. Licha ya kuwa tamu, tende haziongezi kiwango cha sukari mwilini, hivyo zinaweza kutumika kama mbadala wa sukari.
7. Huimarisha Mifupa na kuondoa maumivu ya mara kwa mara ya mifupa kutokana na kuwa na madini ya chuma, na potassium kwa wingi.
8. Tende ina msaada mkubwa kwa mama mjamzito, humuongeza nguvu, na hazina madhara kiafya kwa mtoto. Pia husaidia kupata uzazi salama.
9. Ulaji wa tende kwa wingi husaidia kuongeza mwili kwa wale waliokonda kupita kiasi. Hivyo hushauriwa kula tende kupita kiasi kama huhitaji kuongeza mwili
Mwanamke kuamka mapema asubuhi kunapunguza uwezekano wa kupata saratani ya matiti
Updated at: 2024-05-25 10:35:09 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kuamka asubuhi na mapema hupunguza uwezekano wa mwanamke kupata saratani ya matiti.
Kulingana na shirika la habari la BBC,wataalamu wa chuo kikuu cha Bristol nchini Uingereza wamewafanyia tathmini wanawake 400,000 na kutambua kuwa sio rahisi kwa mwanamke anaeamka asubuhi na mapema kupata saratani ya matiti.
Utafiti huo umeoneysha kuwa wanawake wanaoamka wamechelewa wana hatari kubwa ya kupata ugonjwa huo ukilinganisha na wale wanaoamka wamechelewa.
Utafiti wa hapo awali ulionyesha kuwa kufanya kazi mpaka usiku wa manane kunaongeza hatari ya kupata saratani.
Matokeo ya utafiti huo yatawasilishwa kwenye Mkutano wa Taifa wa Taasisi ya Utafiti wa Saratani huko Glasgow.
Updated at: 2024-05-25 10:37:51 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Matunda yote yana faida mwilini kiafya lakini matunda yanatofautiana kifaida. Zifuatazo ni faida za kula matunda ya aina Mbalimbali;
FAIDA ZA TANGO
1. Kuzuia kisukari, kuboresha mfumo wa damu na kuondoa kolesteroli mwilini. 2. Chanzo kikubwa cha Vitamin B. 3. Kusaidia kutunza ngozi. 4. Kuongeza maji mwilini. 5. Kukata hangover. 6. Kuimarisha mmeng'enyo wa chakula mwilini. 7. Kuzuia saratani mwilini. 8. Kusaidia kupungua uzito. 9. Kuondoa maumivu na kuboresha viungo vya mwili. 10. Kuondoa harufu mbaya ya kinywa.
FAIDA ZA PAPAI
1. Kuua na kuondoa mazalia ya minyoo mwilini. 2. Kusaidia kutibu vidonda vya tumbo. 3. Kuboresha mmeng’enyo wa chakula. 4. Majani yake huleta ahueni kwa wagonjwa wa saratani. 5. Kupunguza uvimbe (anti-inflammatory). 6. Kuboresha misuli na neva mwilini. 7. Kusaidia kumeng’enya protini. 8. Kuboresha kinga ya mwili. 9. Kuboresha macho. 10. Kuboresha mfumo wa hewa
FAIDA ZA UBUYU
1. Kuzuia uhalibifu na mikunjo ya ngozi. 2. Kusaidia katika kupunguza uzito wa mwili. 3. Kuimarisha moyo. 4. Kusafisha ini na kuondoa sumu. 5. Kiwango kikubwa cha vitamin C. 6. Chanzo cha madini ya Calcium. 7. Kuimarisha kinga ya mwili. 8. Kuimarisha figo. 9. Kuimarisha mifupa na meno. 10. Kuimarisha mfumo wa fahamu
FAIDA ZA EMBE
1. Kupunguza kiwango cha asidi mwilini. 2. Kuboresha mmeng’enyo wa chakula. 3. Kurekebisha kiwango cha insulin. 4. Kuboresha macho. 5. Kusafisha damu. 6. Kuboresha ngozi. 7. Kuzuia saratani. 8. Kuimarisha kinga mwilini. 9. Kutibu joto kiharusi (heat stroke). 10. Kupunguza kiwango cha kolesteroli.
FAIDA ZA NANASI
1. Chanzo kikubwa cha vitamin A. 2. Kusaidia kumeng’enya chakula. 3. Inarekebisha mapigo ya moyo. 4. Kuimarisha mifupa ya mwili. 5. Ina kiwango kidogo cha kalori. 6. Inasaidia kuzuia mafua na homa. 7. Kuimarisha mfumo wa kinga. 8. Chanzo cha vitamin C. 9. Inapunguza uvimbe. 10. Kupunguza spidi ya kuzeeka kwa seli mwilini
FAIDA ZA NJEGERE
1. Kuzuia saratani ya tumbo. 2. Kurekebisha kiwango cha sukari kwenye damu. 3. Chanzo kizuri cha protini. 4. Kuboresha ufanyaji kazi wa ini. 5. Ina kiwango kidogo cha kalori. 6. Kuboresha kinga ya mwili. 7. Inaleta nguvu mwilini. 8. Ina virutubisho vya nyuzi nyuzi. 9. Inazuia kuzeeka haraka. 10. Imejaa virutubishi vingi muhimu mwilini.
FAIDA ZA PILIPILI HOHO
1. Husaidia kupunguza uzito. 2. Kuboresha mzunguko wa damu. 3. Inapunguza kolesteroli mwilini 4. Kuzuia shinikizo la damu. 5. Ina kiwango kidogo cha kalori. 6. Nzuri kwa kuboresha macho. 7. Kuimarisha mfumo wa kinga. 8. Inatibu anemia. 9. Inazua saratani. 10. Kuboresha moyo.